Marekani yathibitisha kufanya shambulizi la anga dhidi ya Al-Shabaab nchini Somalia
Kituo cha jeshi la Marekani barani Afrika AFRICOM kimethibitisha kuwa kwa kushirikiana na majeshi ya Somalia na Umoja wa Afrika na washauri wa Marekani, jeshi hilo lilifanya shambulizi la anga dhidi ya kundi la Al-Shabaab ikiwa sehemu ya mapambano dhidi ya ugaidi.
Jeshi hilo la AFRICOM limetoa taarifa ikisema, shambulizi hilo lilifanywa Januari 7 dhidi ya kundi hilo la kigaidi lenye uhusiano na kundi la Al-Qaeda katika wilaya Gaduud iliyoko kaskazini ya Kismayu, kusini mwa Somalia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |