• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (22 Aprili-28 Aprili)

    (GMT+08:00) 2017-04-28 20:07:24

    Mapigano ya kikabila yasababisha vifo vya watu 20 Kasai ya Kati nchini DRC

    Watu 20 wameuawa katika mapigano ya kikabila katika jimbo la Kasai ya Kati nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

    Jeshi la kulinda amani la Umoja wa Mataifa nchini humo MUNUSCO limesema mauaji hayo yalifanyika tarehe 19 mwezi huu wa Aprili kati ya makabila ya Lulua-Luba na Chowe-Pende.

    Ripoti zinasema kuwa watu wote waliouawa ni kutoka kabila la Chowe-Pende.

    Jimbo la Kasai ya Kati limeendelea kushuhudia machafuko tangu mwaka uliopita kati ya wanajeshi wa serikali na waasi wa Kamwina Nsapu.

    Wakati uo huo, maafisa wa Umoja wa Mataifa wamezindua mpango wa kukusanya Dola Milioni 65.4 kuwasaidia watu waliokimbia makwao katika jimbo hilo kwa sababu ya ukosefu wa usalama.

    Umoja wa Mataifa unasema kuwa zaidi ya watu laki 7 wanahitaji misaada ya kibinadamu kama chakula, makaazi na maji.


    1 2 3 4 5 6 7
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako