• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (10 Julai-14 Julai)

    (GMT+08:00) 2017-07-14 19:26:47

    Rais wa zamani Abdulaye Wade arejea nyumbani kuwania ubunge

    Rais wa zamani wa Senegal Abdulaye Wade amerejea nyumbani jijini Dakar kushiriki uchaguzi wa wabunge ambao umepangwa kufanyika tarehe 30 mwezi Julai mwaka huu, ambapo pia anagombea kama mbunge.

    Wade mwenye umri wa miaka 91 amesema anaamini kuwa lengo lake kugombea ubunge ni kwa sababu anataka kuendelea kuwatetea raia.

    Katika kampeni yake, ameshutumu serikali ya rais Macky Sall iliyoko madarakani kwa kuchochea kesi inayomkabili mtoto wake Karim Wade, ambaye anakabiliwa na kesi ya kujitajirisha kinyume cha sheria.

    Wade, aliongoza Senegal kwa miaka 12 kati ya mwaka 2000 hadi mwaka 2012 na kwenda kuishi nchini Ufaransa.

    Mwaka 2012, aliwania urais kwa muhula wa wa tatu lakini akashindwa baada raia wa nchi hiyo kumchagua kiongozi wa sasa Macky Sall.

    1  2  3  4  5  6  7  8  9  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako