• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii ( 7 Agosti-11 Agosti)

    (GMT+08:00) 2017-08-11 18:20:21

    Mamia ya raia wakimbia mapigano Saudia

    Eneo la Mashari ya Saudi Arabia linaendelea kukumbwa na mapigano kati ya jeshi la nchi hiyo na watu wenye silaha. Maafisa kadhaa wa polisi na watu waliojihami wameuawa katika mpigano ya hivi karibuni.

    Mamia ya wakazi wa eneo hilo wamelazimika kuyatoroka makazi yao kutokana na mapigano yaliyoanza tangu wiuki kadhaa zilizopita.

    Vikosi vya usalama vimelenga maeneo ya kale ya Awamiya, ambayo wanasema ni sehemu wanakojificha wapiganaji wa Shia.

    Maafisa wa utawala wanataka kulibomoa eneo hilo la kale lenye miaka 200 katika operesheni ilioanzishwa mnamo mwezi Mei.

    Mji wa Awamiya ni nyumbani anakotoka Sheikh Nimr al-Nimr, kiongozi wa kidini mwenye ushawishi anayewaunga mkono waandamanaji wa Kishia, ambaye aliuawa mwaka mmoja na nusu uliopita.

    1  2  3  4  5  6  7  8  9  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako