• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (2 Oktoba-6 Oktoba)

    (GMT+08:00) 2017-10-06 18:58:25

    Watu 20 wauwawa na kimbunga Nate Amerika ya Kati

    Kimbunga Nate kimewaua watu zaidi ya 20 nchini Costa Rica, Nicaragua na Honduras huku kikielekea kaskazini upande wa Marekani.

    Hali ya dharura imetangazwa katika mataifa kadha ya Amerika ya Kati ambapo watu zaidi ya 20 bado hawajulikani walipo.

    Kimbunga hicho kimesababisha mvua kubwa, maporomoko ya ardhi na mafuriko.

    Barabara nyingi hazipitiki, madaraja yameporomoka na pia kimesababisha uharibifu mkubwa kwenye nyumba za watu na majengo.

    Nchini Costa Rica, watu karibu 400,000 hawana maji na maelfu wengine wameachwa bila makao na wanalala kwenye vyumba vya muda.

    Watu zaidi ya sita wamethibitishwa kufariki katika taifa hilo.

    Watu wengine 11 waliuawa kimbunga hicho kilipokuwa kinaelekea kaskazini na kufika Nicaragua.

    Watu watatu wameuawa nchini Honduras na kuna watu kadha ambao hawajulikani waliko.

    Nchini Costa Rica, safari zote za treni zimesitishwa na safari kadha za ndege pia zimefutwa.

    Mbuga kadha za taifa ambazo ni maarufu kwa watalii pia zimefungwa kama tahadhari.

    Kimbunga hicho pia kimesababisha uharibifu mkubwa kwenye miundo mbinu Nicaragua.

    Watabiri wanasema kimbunga Nate kitaimarika na kuwa kimbunga cha ngazi 1 kabla ya kufika tena ardhini pwani ya kusini mwa Marekani siku ya Jumapili.

    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako