• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii ( 2 Desemba-8 Desemba)

    (GMT+08:00) 2017-12-08 20:27:13

    Kiongozi wa upinzani Kenya aonywa dhidi ya kuapishwa

    Mwanasheria mkuu wa Kenya Prof Githu Muigai amesema jaribio lolote la kumuapisha kiongozi mwingine wa Kenya litakuwa ni uhaini wa hali ya juu.

    Prof Muigai amesema hayo huku kiongozi wa upinzani nchini humo Raila Odinga akisisitiza kwamba ataapishwa kuwa rais Jumanne wiki ijayo.

    Bw Odinga alitangaza mwezi uliopita kwamba ataapishwa na Mabunge ya Wananchi ambayo yalipendekezwa na muungano wa upinzani National Super Alliance (Nasa).

    Ingawa hakumtaja mtu yeyote, Prof Muigai, akiwahutubia wanahabari Nairobi, alisema shughuli hama hiyo ya kumuapisha kiongozi ambaye hajatangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (IEBC) haina msingi wowote kikatiba na kwamba itakuwa "bure na batili".

    "Sheria za jinai za Jamhuri ya Kenya zinazungumzia shughuli kama hiyo kuwa uhaini wa hali ya juu," amesema.

    "Wanaoshiriki watakuwa wanajihusisha katika uhaini wa hali ya juu, pamoja na wote wanaofanikisha shughuli kama hiyo."

    Adhabu ya kosa la uhaini kwa mujibu wa sheria za Kenya ni kifo.

    Prof Muigai amesema Mabunge ya Wananchi ambayo yanaundwa na Nasa pia ni kinyume cha sheria.

    Kufikia sasa, mabunge 12 ya majimbo, ikiwa ni pamoja na Mombasa, ambayo yanaongozwa na magavana wa muungano wa Nasa tayari yamepitisha azimio la kuundwa kwa mabunge hayo ya wananchi.

    Kenya kwa jumla ina majimbo 47.

    Nasa ilipendekeza kuundwa kwa mabunge hayo kama njia ya kushinikiza mageuzi nchini humo baada ya kususia uchaguzi wa marudio uliofanyika tarehe 26 Oktoba.

    Rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi wa uchaguzi huo ambao ulisusiwa na upinzani.

    Alipata kura 7.5 milioni, sawa na asilimia 98 ya kura zilizopigwa ingawa waliojitokeza walikuwa asilimia 39.

    Bw Kenyatta aliapishwa kuwa rais tarehe 28 Novemba kwenye sherehe ambayo upinzani ulisusia.

    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako