• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (March 24-March 30)

    (GMT+08:00) 2018-03-30 18:47:26

    Abiy Ahmed achaguliwa kuwa waziri mkuu mpya Ethiopia

    Muungano wa vyama vinavyounda Serikali nchini Ethiopia vimemchagua Abiy Ahmed kutoka kwenye kabila kubwa la Oromom uteuzi ambao umetoa fursa ya yeye kuwa waziri mkuu.

    Kama kiongozi wa chama cha Ethiopian Revolutionary Democratic Front, Abiy anatarajiwa kuchukua madaraka kutoka kwa Hailemariam Desalegn ambaye alitangaza kujiuzulu mwezi uliopita katika uamuzi wa kushtukiza baada ya miaka miwili ya maandamano kuipinga Serikali.

    Abiy atakuwa waziri mkuu wa kwanza kutoka kabila la Oromo katika kipindi cha miaka 27 ya utawala wa chama cha EPRDF ambacho tangu kuingia kwake madarakani kimefanikiwa kubadili uchumi wa taifa hilo.

    Licha ya mvutano wa kikabila wananchi wengi wa Ethiopia wana imani kuwa Abiy atabadili uelekeo wa chama tawala ambacho kilichukua madaraka mwaka 1991 kutoka kwa utawala wa kijeshi.

    Mwaka 2015 hasira dhidi ya chama tawala iliongezeka na kusababisha wanaharakati wa eneo la Oromo kuanzisha maandamani ya kuipinga Serikali maandamano ambayo yameshuhudia mamia ya watu wakipoteza maisha.

    Kabila la pili kwa ukubwa nchini humo la Amharas baadae walijiunga kwenye maandamano ambayo hata hivyo lilijiondoa baada ya Serikali kutangaza miezi 10 ya hali ya hatari.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako