• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Aprili 28-Mei 4)

    (GMT+08:00) 2018-05-04 17:45:34

    Watu 24 wauwawa Jamhuri ya Afrika ya kati

    Rais wa Jamhuri ya Afrika ya kati Faustin Archange Touadera ametangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo vya watu wasiopungua ishirini na wanne waliouawa katika mapigano kati ya wapiganaji wenye silaha na vikosi vya serikali.

    Mapigano hayo yalitokea katika mji mkuu wa nchi hiyo Bangui ambapo kanisa Notre Dame lilishambuliwa pia.

    Tume ya umoja wa Mataifa nchini humo MINUSCA imesema imeimarisha doria kwenye mji mkuu Bangui na hasa wilaya ya PK5 ambayo imekuwa kitovu cha vurugu za kidini na umiliki wa maeneo wa makundi ya wapiganaji.

    Mapigano haya yanazusha maswali zaidi kuhusu uimara wa serikali ya nchi hiyo na uwepo wa vikosi vya MINUSCA.

    Machafuko nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati yamesababisha vifo vya watu wengi na maelfu wengine kulazimika kuyahama makazi yao.

    Wadadisi wanasema kuwa vita hivyo vinachochewa kidini, lakini kuna mwingiliano wa kisiasa.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako