Nigeria yapiga kura ya urais
Raia wa Nigeria wanapiga kura leo kuchangua bunge na rais mpya.
Kuna wagombea 72 wa kiti cha urais, lakini washindani wakuu ni Atiku Aboubakar na rais wa sasa Muhammadu Buhari ,
Atiku Aboubakar anagombea kiti hicho kwa mara ya nne sasa.
Anasifika kuwa mfanyabiashara mzuri, lakini suala la Rushwa wakati alipokua makamu wa rais linatia doa jitihada zake.
Naye rais wa sasa alichaguliwa mwaka 2015 baada ya kuahidi kutokomeza kundi la Boko Haram, kupambana dhidi ya rushwa na kuimarisha uchumi.
Wafuasi wa Bwana Buhari wanahoji kwamba ametimiza ahadi zake alizotoa wakati wa kampeni kama vile kukabiliana na ufisadi na kukabiliana na kundi la Boko haram.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |