Museveni kugombea tena Urais
Mahakama ya juu nchini Uganda imethibitisha uamuzi wa mahakama ya katiba ya nchi hiyo kuidhinisha mabadiliko ya katiba yaliondoa ukomo wa umri wa kugombea urais.
Kesi hiyo ilifunguliwa katika mahakama hiyo na wapinzania wa rais wa nchi hiyo Yoweri Musevenia mabo wanataka kumzuia kugombea uraisi kwa awamu ya sita.
Hata hivyo, majaji wanne walipinga hoja za rufaa hiyo huku wanne wakikubaliana nayo.
Jaji Mkuu wa Uganda Bart Katureebe alitangaza kuwa "rufaa hii imeshindwa" kutokana na zaidi ya nusu ya majaji wa mahakama hiyo kuipinga. Mwezi Julai mwaka 2018, Majaji wanne kati ya watano wa jopo la majaji ya Katiba ya nchi hiyo waliamua kuwa mabadiliko hayo ya katiba ni halali.
Awali umri wa mwisho kwa kugombea ulikuwa ni miaka 75.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |