• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Juni 1-Juni 7)

    (GMT+08:00) 2019-06-07 16:43:34
    Zimbabwe yaanza mazungumzo na mataifa ya EU kuiondolea vikwazo

    Zimbabwe na umoja wa Ulaya zimeanza mazungumzo katika juhudi za kuondolewa vikwazo vilivyowekewa nchi hiyo.

    Mabalozi kutoka nchi za umoja wa Ulaya walioko Zimbabwe wamekutana na wawakilishi wa Serikali katika awamu ya kwanza ya mfululizo wa mazungumzo yaliyopangwa kufanyika baina ya pande hizo mbili kujaribu kumaliza miongo kadhaa ya vikwazo vya kiuchumi kwa Zimbabwe.

    Umoja wa Ulaya uliondoa sehemu kubwa ya vikwazo vya kiuchumi kwa nchi ya Zimbabwe mwaka 2014 lakini imekuwa haitoi msaada wa kifedha kwa Serikali.

    Hatua hii imekuja, baada rais wa Marekani Donald Trump, mapema mwaka huu kuongeza vikwazo vya muda wa mwaka mmoja zadi kwa taifa hilo la Kusini mwa Afrika.

    Uongozi wa rais Trump unasema kuwa, sera za serikali ya rais Emmerson Mnangagwa bado ni hatari kwa sera yake ya mambo ya nje.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako