• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Juni 1-Juni 7)

    (GMT+08:00) 2019-06-07 16:43:34

    Ebola yaathiri watu 2,000 DRC

    Zaidi ya watu 2,000 wameripotiwa kuugua ugonjwa wa Ebola nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika kipindi cha miezi 10, maafisa wameeleza.

    Theluthi mbili walikua kwenye hali mbaya zaidi, wizara ya afya imeeleza.

    Mlipuko wa ebola ni wa pili kwa ukubwa nchini DRC,kukiwa na ripoti ya kutokea maambukizi mapya wiki za hivi karibuni.

    Lakini wafanyakazi wa afya wamekua wakipata vikwazo vya kutoaminika na machafuko nchini humo.

    Watu wengine hawawaamini watoa huduma za afya, hivyo hufanya watu wenye dalili za ugonjwa huo kukwepa matibabu, hali hii inawia vigumu kuzuia kuenea kwa virusi vya ebola.

    Ingawa zaidi ya watu 1,300 wamepoteza maisha tangu mwezi Agosti, Shirika la misaada la Oxfam linasema linakutana na watu kila siku ambao hawaamini kama kuna virusi vya ebola.

    Kati ya mwezi Januari na Mei kulikua na matukio 40 ya mashambulizi dhidi ya vituo vya afya, Hata hivyo machafuko yamepungua majuma ya hivi karibuni.

    Shirika la afya duniani WHO, limesema kuwa hatari ya kusambaa zaidi si kubwa sana, lakini inawezekana ugonjwa huo kuingia nchi jirani.

    Mlipuko wa ebola mara nyingi husambaa haraka na kuathiri idadi ndogo ya watu.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako