• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Decemba 28-Januari 3)

    (GMT+08:00) 2020-01-03 18:37:17

    Nzige Wavamia eneo la Kaskazini mwa Kenya na kuharibu mimea

    Kuna hofu ya baa la njaa kulikumba eneo la kaskazini mwa Kenya baada ya eneo hilo kuvamiwa na mamilioni ya nzige ambao chimbuko lake linaaminika kuwa Yemen kisha wakahamia Ethiopia na Somalia. Zaidi ya ekari 70,000 ya mashamba Ethiopia na Somalia yameathiriwa na nzige hao.

    Kinachowashangaza wengi ni hatua ya maafisa wa usalama kuamua kutumia vitoa machozi na hata kupiga risasi angani ili kuwatawanya nzige hao.

    Vile vile wenyeji wa maneo yaliyoathirika waliungana na maafisa wa polisi kwa kupiga mayowe na kutumia vifaa mbalimbali kama njia za kuwatfukuza nizge hao.

    Tayari serikali imetoa helikopta moja itakayotumiwa kunyunyizia dawa na kuwaangamiza nzige hao.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako