• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Decemba 28-Januari 3)

    (GMT+08:00) 2020-01-03 18:37:17

    Orodha ya matajiri duniani

    Mwanzilishi wa Kampuni ya Kimataifa ya Teknolojia ya Amazon, Jeff Bezos anaongoza katika orodha ya Matajiri duniani japokuwa amepoteza Dola za Marekani Bilioni 10 kwa mwaka mmoja.

    Kwa mujibu wa orodha iliyotolewa na 'Bloomberg Billionaire Index', hadi kufikia Januari 02, 2020, Jeff alikuwa na utajiri wa Dola za Marekani Bilioni 115 akifuatiwa kwa karibu na Mwanzilishi wa Microsoft, Bill Gates mwenye utajiri wa Dola za Marekani Bilioni 113.

    Jeff alikuwa anatarajiwa kupoteza nafasi ya kwanza baada ya kupeana talaka na aliyompatia Mke wake, Mackenzie Bezos ambapo sasa Jeff anamiliki 75% ya hisa za Amazon.

    Mackenzie Bezos (aliyekuwa Mke wa Jeff Bezos) anashika nafasi ya 25 katika orodha hiyo huku Mwanzilishi wa Mtandao wa Fcebook, Mark Zuckerberg akiwa nafasi ya tano.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako