Cipriano Cassama, ajiuzulu Urais baada ya siku moja tu kupita tangu kukaa madarakani
Cipriano Cassama ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya Urais, Guinea-Bissau baada ya kukaa madarakani kwa siku moja, akisema maisha yake yalikuwa hatarini.
Cipriano Cassama alichaguliwa na wabunge kuwa rais wa mpito baada ya chaguzi zilizo susiwa mwezi Disemba.
"Leo hii maisha yangu yamekuwa hatarini, familia yangu imekuwa hatarini, maisha ya watu wengi yamekuwa hatarini pia, na ndiyo maana nimeamua kujiuzulu." amesema
Hatua hii ni pamoja na ukweli kuwa Jenerali wa jeshi wa zamani Umaro Cissoko Embaló tayari alikwisha apishwa kuwa rais katika hoteli mji mkuu wa nchi hiyo, Bissau.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |