• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Aprili 25-Mei 1)

    (GMT+08:00) 2020-05-01 19:54:56
    IRC yasema watu bilioni 1 huenda wakaambukizwa Corona Duniani

    Watu bilioni moja huenda wakaambukizwa virusi vya corona kote duniani na mambo pengine yabadilike, nchi zisizojiweza zinahitaji usaidizi wa haraka, Shirika la kutoa msaada limeonya.

    Kamati ya Shirika la Kimataifa la Kutoa Misaada (IRC) limesema kwamba msaada wa kifedha na kibinadamu vinahitajika kusaidia kupunguza kasi ya usambaaji wa virusi vya corona.

    Shirika hilo limesema nchi zinazokabiliwa na vita kama Afghanistan na Syria zinahitaji msaada wa dharura wa kifedha kuzuia mlipuko wa ugonjwa wa corona.

    Kumekuwa na zaidi ya watu milioni 3 walioambukizwa ugonjwa wa Covid-19 kote duniani huku zaidi ya vifo 200,000 vikithibitishwa, kulingana na Chuo Kikuu cha Johns Hopkins Marekani.

    Ripoti ya shirika hilo, ambayo inazingatia data za Shirika la Afya Duniani (WHO) na chuo cha Imperial College London, ilikadiria kwamba kunaweza kuwa na maambukizi kati ya milioni 500 na bilioni 1 kote duniani.

    Pia imesema kwamba huenda idadi ya vifo ikawa ni milioni 3 katika nchi zinazokumbwa na migogoro na zisizokuwa na uthabiti.


    1  2  3  4  5  6  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako