• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Juni 13-Juni19 )

    (GMT+08:00) 2020-06-19 20:44:11
    Matangazo ya kampeni ya Trump yaondolewa na Facebook 'kwa kuchochea chuki'

    Mtandao wa kijamii wa Facebook umeondoa mtandaoni matangazo ya kampeni ya rais Donald Trump kwa kutumia alama zilizokuwa za utawala wa kinazi wa Ujerumani.

    Facebook imesema tangazo lililolengwa lilikuwa na alama ya pembe tatu nyekundu kama iliyotumika na utawala wa kinazi kuwatambua wapinzani wao kama wakomunisti.

    Matangazo hayo ni sehemu ya kampeni ya Trump kwa uchaguzi wa Novemba mwaka huu.

    Timu ya kampeni ya Trump imesema kuwa tangazo hilo lilikuwa linakilenga kikundi cha wanaharakati wa mrengo wa kushoto antifa, ambacho wanadai kinatumia nembo hiyo.

    Facebook inadai matangazo hayo yanaenda kinyume na sera yake ya chuki ya kupangwa.


    1  2  3  4  5  6  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako