• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Oktoba 10-Oktoba 16)

    (GMT+08:00) 2020-10-16 16:53:39
    Makasisi wa kikatoliki washtakiwa kwa tuhuma za unyanyasaji wa kingono

    Mapadre wawili wa Kanisa Katoliki mapema wiki hii walifikishwa mahakamani mjini Vatcan kwa madai ya unyanyasaji wa kingono. Kasisi wa kwanza kwa jina Gabriele Martinelli, aliye na umri wa mika 28, anashutumiwa kumnyanyasa kingono mvulana aliyekuwa akitumikia kwenye madhabahu ya kanisa kati ya mwaka 2007 na 2012.

    Mwingine ni Padre Enrico Radice, mwenye umri wa miaka 72, ambaye anashtakiwa kwa kuficha madai ya unyanyasaji huo wakati alipokuwa mkuu wa shule ya theolojia ambako tukio hilo linadaiwa kufanyika.

    Huku makasisi kadhaa wamekwisha kabiliwa na mashitaka kote duniani, Vatcan haijawahi kuendesha kesi inayohusiana na unyanyasaji wa kingono katika mahakama yake. Hao ndio makasisi wa kwanza kuwahi kushtakiwa katika mji huo wa Vatican


    1  2  3  4  5  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako