11: Mikoa ya Xinjiang na Tibet

Dini mkoani Tibet

Dini ya kibudha ya kitibet na mahekalu ya wa-lama

Dini ya kibudha ya kitibet imeenea kwenye sehemu ya Tibet na Mongolia ya ndani nchini China, wenyeji wa huko waliita dini hiyo kuwa ni "dini ya lama", hii ni dini ya kibudha iliyoenea Tibet kutoka India na sehemu za ndani za China ambayo iliunganishwa na dini za kale za huko na kuwa dini yenye umaalum wa kitibet.

Kutokana na athari ya dini ya kibudha ya kabla ya wahan la China na dini ya kibudha ya India, mahekalu ya dini ya kibudha ya kitibet mengi yalijengwa kwa mtindo wa jengo la kifalme la kabila la wahan tena kuonesha mtindo wa kitibet, kwa kawaida, mahekalu hayo ni makubwa sana yenye taadhima, mapaa ya majengo huchongwa nakshi na kuchorwa picha ambayo yanaonekana ya kupendeza sana. Kwa mfano, Kasri la Budara la Lahsa, Hekalu la Drepung na Hekalu ya Tar la Qinghai yote ni majengo mazuri ya zama za kale.

Ujenzi wa mahekalu ya Tibet pia hutilia maanani zaidi kwa kuonesha taswira, ajabu na miujiza ya dini ya kibudha ya kitibet. Mahekalu ya kawaida huwa na ukumbi mkubwa na mrefu wa kuabubu sanamu za budhaa, ndani kupambwa na mapazia ya kidini ya rangi mbalimbali, nguzo za ukumbini hupambwa kwa mazulia za rangi, ndani kuna giza kidogo, hivyo watu wakiingia huko hujisikia ajabu ya dini.

Desturi za kidini za Raia wa Tibet

Watu wa Tibet wana uelewa wa kutosha wa kuamini dini. Watu wengi wa makabila ya watibet, wabenba, waloba na wanaxi wa mkoa unaojiendesha wa Tibet ni waumini wa dini ya kibudha ya kitibet, pia kuna waumini wengi wa dini ya kiislamu na kikatoliki. Hivi sasa mkoani Tibet kuna sehemu zaidi ya 1700 za kufanyika shughuli za dini ya kibudha ya kitibet, watawa wa kiume na kike wanaokaa katika mahekalu wamefikia elfu 46; kuna misikiti minne, waumini wa dini ya kiislamu zaidi ya 3000; kanisa moja ya kikatoliki, waumini zaidi ya 700.

Watu wa kabila la watibet na makabila mengine madogo madogo mkoani Tibet wana haki na uhuru wa kuishi maisha na kufanya shughuli za jamii kwa kufuata desturi na mila zao wenyewe. Wanapodumisha desturi na mila yao ya jadi katika mavazi, chakula na makazi ya makabila yao, pia wamejifunza desturi mpya zinazoonesha ustaarabu wa zama za hivi sasa na maisha mazuri katika malazi na chakula pamoja na shughuli za kufunga ndoa au mazishi. Watu wa mkoa wa Tibet wanaendelea kufanya shughuli nyingi za jadi kama vile za kusherehekea mwaka mpya wa jadi wa Tibet, sikukuu ya mavuno na sikukuu ya Xuedun pamoja na shughuli nyingi za kidini. Pia watibet wa hivi sasa pia wanafanya shughuli mpya za aina mbalimbali za China na ng'ambo.


1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13