• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii ( Agusti 13-Agusti 19)

    (GMT+08:00) 2016-08-19 18:47:32

    Serikali ya DRC yatangaza amri ya kutotoka nje usiku Beni na Butembo

    Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetangaza Alhamisi hii, Agosti 18, amri ya kutotoka nje usiku katika miji ya Beni na Butembo, mashariki mwa nchi hiyo, baada ya maandamanoya Jumatano wiki hii dhidi ya serikali.

    Wakazi wa miji hiyo wametakiwa kutotoka nje kuanzia saa moja usiku gadi saa kumi na mbili asubuhi. Tangazo hili limetolewa na Naibu Waziri Mkuu mwenye dhamana ya Mambo ya Ndani, Evariste Boshab. Hatua ambayo haikuwaridhisha wafanyabiashara. Wafanyabiasha katika mji wa Beni waliamua Alhamisi hii kufunga maduka yao katika barabara kuu ya Nyamwisi. Wafanyabiashara wanaomba kuachiwa huru kwa waandamanaji wanaozuiliwa.

    Katikati mwa mji wa Beni, maduka yalifungwa Alhamisi hii Agosti 18 kwenye barabara kuu ya Nyamwisi ambapo ni moja ya meneo kulikofanyika maandamano ya Jumatano. Wafanyabiashara wameeleza kwamba bado wanaomboleza wahanga wa tukio hilo.


    1 2 3 4 5 6 7
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako