Kongamano la nchi za Kiarabu linalolenga kupinga ugaidi lafanyika nchini Sudan
Wiki hii viongozi wan chi za Kiarabu wamekongamana nchini Sudan mjini Khartoum, Sudan na kujadili kuimarisha ushirikiano wa usalama na kushirikiana katika kupambana na ugaidi.
Kongamano hilo liliandaliwa kwa pamoja na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na wizara ya mambo ya nje ya Sudan. Makamu wa rais wa Sudan Bw. Bakri Hassan Saleh amesema, Sudan siku zote inazingatia kupambana na ugaidi, na katika miaka ya karibuni, nchi hiyo ilichukua hatua za kupinga ugaidi na kuzuia ugaidi kupenya nchini humo, hasa kwenye sehemu ya kaskazini ya Darfur karibu na Libya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |