3. Ajali ya kugongana kwa treni iliyotokea Alhamis kwenye kituo cha Hoboken cha jimbo la New Jersey nchini Marekani, imesababisha kifo cha mtu mmoja na wengine zaidi 100 kujeruhiwa, chanzo cha ajali hiyo bado kinaendelea kuchunguzwa.
Mbali na hapo kuhusiana na ajali ya kupinduka kwa meli iliyobeba wahamiaji haramu iliyotokea wiki iliyopita kwenye eneo la Bahari ya Mediterranean hadi sasa idadi ya watu waliofariki imefikia 202. Habari kutoka tovuti ya gazeti la Piramidi la Misri zinasema abiria wengi zaidi ni wamisri, na wengine ni wahamiaji haramu kutoka nyingine za Afrika. Tarehe 21 meli iliyobeba wahamiaji haramu 600 hivi ilipinduka kwenye eneo la Bahari ya Mediterranean. Hadi sasa watu 163 wameokolewa, na wengine wengi hawajulikani walipo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |