• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Novemba 5-Novemba 11)

    (GMT+08:00) 2016-11-11 19:21:42

    Rais Jacob Zuma aepuka kura ya kutokuwa na imani naye

    Kura ya kutokuwa na imani dhidi ya rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma imeshindwa kufaulu katika bunge licha ya madai ya hivi karibuni ya ufisadi.

    Uchunguzi wa tume ya kukabiliana na ufisadi nchini humo wiki iliopita ulizua madai ya utovu wa nidhamu dhidi ya rais Zuma.

    Chama cha cha rais Zuma ANC kina wabunge wengi katika bunge na mswada huo wa upinzani ulishindwa kwa kura 214 dhidi ya 126.

    Hii ni kura ya tatu ya kutokuwa na imani naye iliowasilishwa bungeni katika kipindi kisichozidi mwaka mmoja.

    Uchunguzi uliofanywa na tume ya kukabiliana na ufisadi nchini humo ulisema kuwa jopo la majaji linafaa kubuniwa ili kuchunguza madai ya uhalifu katika serikali ya Zuma.

    Uchunguzi huo ulipata ushahidi kwamba familia ya Gupta ilio na uhusiano mkubwa na rais Zuma huenda ilikuwa na ushawishi mkubwa katika uteuzi wa baraza la mawaziri.

    Zuma na familia hiyo wamekana kufanya makosa yoyote.


    1 2 3 4 5 6 7 8
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako