• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (14 Oktoba-20 Oktoba)

    (GMT+08:00) 2017-10-20 17:27:55

    Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, aamuru kuimarisha kikosi cha kulinda amani CAR

    Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, ameamuru kuimarisha kikosi cha kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (Minusca) kwa kuongeza idadi ya askari 900 kutokana na kuzuka upya kwa machafuko nchini humo.

    Katika ripoti iliyowasilishwa siku ya Jumanne kwa Baraza la Usalama, Bw. Guterres anasema Jamhuri ya afrika ya Kati inatisha kwa sasa .

    Wakati huo huo Umoja wa Mataifa unasema watoto nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati wanakabiliwa na baa la njaa na kusababisha kupoteza maisha.

    Hatua hii imekuja baada ya machafuko kuendelea kushuhudiwa nchini humo na kusababisha wafanyakazi wa misaada ya kibinadamu kukimbia nchini humo.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako