• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (14 Oktoba-20 Oktoba)

    (GMT+08:00) 2017-10-20 17:27:55
     

    IGAD yasema itafufua mazungumzo ya amani ya Sudan Kusini yaliyokwama ndani ya miezi miwili

    Shirika la maendeleo la kiserikali la nchi za Afrika Mashariki IGAD, limesema mkutano wa ngazi ya juu wa kutafuta suluhisho la kisiasa la mgogoro wa Sudan Kusini, utafanyika ndani ya miezi miwili. Mjumbe maalum wa IGAD nchini Sudan Kusini Bw Ismail Wahid, amesema shirika hilo litachambua matokeo ya mawasiliano na makundi yote yanayohusika na mgogoro wa Sudan Kusini na kuweka machaguo ya kufufua mazungumzo hayo. Baraza la mawaziri la IGAD litakutana ili kujadili mapendekezo na machaguo yaliyopo, kabla ya kutangaza rasmi siku ya mkutano, mahali pa kufanyika, watakaohudhuria na ajenda zake. Msemaji wa kundi la SPLA-wapinzani Bw William Gatjiah Deng amekaribisha hatua hiyo, lakini amesema mkutano huo wa ngazi ya juu unatakiwa kuangalia kiini cha mambo yaliyokwamisha makubaliano ya amani ya mwaka 2015.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako