• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (March 10-March 16)

    (GMT+08:00) 2018-03-16 20:20:17

    Moise Katumbi kurejea nchini DRC mwezi Juni

    Kiongozi wa upinzani nchini DRC ambaye sasa anaishi uhamishoni Moise Katumbi Tschapwe, amesema atarejea nchini mwake mwezi Juni mwaka huu.

    Gavana huyo wa zamani wa jimbo la Katanga, ametangaza pia atawania urais mwezi Desemba.

    Akizungumza jijini Johannesburg ambako alikuwa amekutana na wanasiasa wa upinzani, Katumbi amesema watahakikisha wanapigana kuchukua madaraka.

    Mwisho mwa wiki iliyopita, mamia ya wanasiasa wa upinzani walitangaza kumuunga mkono Katumbi kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka huu.

    Mwansiasa huyo wa upinzani amesema lengo lake ya kutaka urais ni kuwasaidia wananchi wa taifa lake kuondokana na umasikini na kutatua changamoto za kiusalama.

    Hata hivyo, ameendelea kutilia shaka, uwezo wa Tume ya Uchaguzi CENI kusimamia Uchaguzi utakaokuwa huru na haki.

    Katumbi alikimbia nchi hiyo kwa sababu za kisiasa baada ya kukabiliwa na mashtaka kuhusu mikataba ya ardhi.

    Mahakama imemhukumu kifungo cha miaka mitatu kutokana na mashtaka hayo ambayo amekuwa akisema yamechochewa kisiasa na rais Joseph Kabila.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako