• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (March 31-Aprili 6)

    (GMT+08:00) 2018-04-06 20:02:35

    Luiz Inacio Lula da Silva kufungwa miaka 12 jela

    Mahakama ya rufaa nchini Brazil imeagiza kuwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Luiz Inacio Lula da Silva, ni sharti aanze kutumikia kifungo chake cha miaka kumi na miwili gerezani, baada ya kupatikana na hatia ya kuhusika na ufisadi.

    Majaji sita kati ya kumi na mmoja wa mahakama ya rufaa walipinga rufaa hiyo huku watano kati yao wakimuunga mkono. Kesi hiyo imezua hali ya wasi wasi wa kisiasa nchini humo.

    Hatia hiyo imetokana na uchunguzi wa muda mrefu wa sakata la rushwa linalojulikana kama ''Operation Car Wash''

    Lula aligundulika kukubali rushwa yenye thamani Euro laki saba na tisini.

    Lula da silva amekua akitarajiwa na watu wengi kusimama kama mgombea asie na ushindani katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi octoba,

    Lakini ndoto hizo zimeisha baada ya mahakama kuu kuamuru mwanasiasa huyo mkongwe aanze kifungo cha miaka 12 gerezani baada ya kukutwa na hatia ya ufisaidi.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako