Kiongozi wa upinzani nchini Sierra Leone achaguliwa rais
Kiongozi wa upinzani nchini Sierra Leone Julius Maada Bio, ameapishwa baada ya kutangazwa na tume huru ya uchaguzi nchini humo kuwa mshindi wa duru ya pili ya uchaguzi uliofanyika Machi 31.
Maada Bio mwanajeshi wa zamani mwenye umri wa miaka 53 ametangazwa kushinda nafasi hiyo kwa asilimia 51.81 dhidi ya mgombea wa chama tawala Samura Kamara aliepata asilimia 48.19.
Hata hivyo mgombea wa chama tawala Samaura Kamara amesema atakata rufaa mahakamani kupinga matokeo hayo yaliotangzwa na tume huru ya uchaguzi ambayo amesema hayakuzingatia malalamiko yake kuhusu dosari zilizojitokeza huku akiwatolea wito wafuasi wake kusalia kuwa watulivu na wenye mshikamano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |