• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Aprili 21-Aprili 27)

    (GMT+08:00) 2018-04-27 19:13:14

    Macron ahitimisha ziara Marekani

    Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amehitimisha ziara yake ya kwanza ya kiserikali nchini Marekani Jumatano wiki hii akihutubia mkutano wa pamoja wa Bunge la Marekani na mkutano na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Georgetown.

    Wakati wa ziara hiyo ya siku tatu, Macron na Rais wa Marekani Donald Trump walizungumzia ushirikiano wa kibiashara, mazingira, Iran na Syria.

    Viongozi hao wawili walikuwepa kuzungumzia tofauti zao na kusisitiza mahusiano ya karibu yaliyoko kati ya nchi hizo na urafiki wao binafsi.

    Wakati wakionyesha urafiki wao kwa maneno na vitendo, Trump na Macron wamekiri kuwa wanashirikiana kuondoa tofauti zao katika mambo kama vile mabadiliko ya hali ya hewa na makubaliano ya nyuklia yaliyofikiwa na Iran.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako