• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Juni 23-Juni 29)

    (GMT+08:00) 2018-06-29 18:47:12

    Watu 15 wafariki katika moto kwa soko Nairobi

    Takriban watu 15 wamefariki alhamisi wiki hii katika moto mkubwa uliokumba soko moja nguo katika mji mkuu wa Kenya Nairobi.

    Zaidi ya watu 70 walijeruhiwa katika moto huo uliotokea katikati ya usiku na kusababisha uharibifu wa mali nyingi.

    Soko hilo la Gikomba ndio soko kubwa zaidi katika mji huo na moto hutokea mara kwa mara.

    Hatahivyo chanzo cha moto huo bado hakijulikani.

    Baadhi ya waathiriwa walichomwa huku wengine wakivuta moshi wenye sumu walipojaribu kuokoa mali yao.

    Maafisa wa hospitalini wanasema kulikuwa na watoto watano miongoni mwa waliofariki.

    Waliojeruhiwa walikimbizwa katika hospitali tofauti mjini humo.

    Soko hilo ni maarufu sana kwa uuzaji wa nguo za mitumba , viatu na mboga, na pia lina maeneo ya kuweka mbao ambayo yaliharibika katika moto huo.

    Soko hilo ni maarufu kwa uuuzaji wa nguo za mitumba viatu na hata mboga, na kuna maeneo ya kuuzia mbao ambayo yameharibiwa kupita kiasi katika moto huo.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako