• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Septemba 1-Septemba 7)

    (GMT+08:00) 2018-09-07 18:54:59

    Viongozi wa Korea Kusini na Korea Kaskazini kukutana mjini Pyongyang baadaye mwezi huu

    Rais Moon Jae-in wa Korea Kusini na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un wanatarajiwa kukutana tarehe 18 hadi 20 mwezi huu mjini Pyongyang.

    Taarifa iliyotolewa na Ikulu ya Korea Kusini imesema, wajumbe kutoka Korea Kusini na Korea Kaskazini wamejadiliana na kufikia makubaliano kuhusu mkutano wa viongozi hao.

    Mkurugenzi wa idara ya usalama ya ikulu ya Korea Kusini Bw. Chung Eui-yong amesema, viongozi hao watatathmini matokeo ya utekelezaji wa azimio la Panmunjom na kujadili mwelekeo wa utekelezaji huo.

    Pia watajadili masuala ya amani na ustawi wa kudumu wa peninsula ya Korea, hasa suala la mpango wa utekelezaji wa kuondoa silaha za nyuklia katika peninsula hiyo.

    Pande hizo mbili zitafanya mkutano wa ngazi ya juu mwanzoni mwa wiki ijayo kujadili maandalizi ya mkutano huo muhimu.


    1  2  3  4  5  6  7  8  9  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako