• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (February 16-February 22)

    (GMT+08:00) 2019-02-22 18:59:17

    Rais wa Somalia azuru Burundi

    Rais wa Somalia Mohamed Farmajo ambaye amekamilisha ziara yake ya siku mbili nchini Burundi amekutana na rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza.

    Ziara hiyo inakuja wakati ujumbe wa Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) unajiandaa kuondoa maelfu ya askari wa Burundi katika kikosi chake mwishoni mwa mwezi huu.

    Baada ya mkutano wao, rais wa Burundi Pierre Nkurunziza na mwenzake wa Somalia Mohamed Farmajo wametoa wito wa mkutano wa haraka wa viongozi wa nchi zinazochangia askari wa AMISOM, nchini Somalia.

    Ombi hilo linahusiana na tangazo la kuondoa maelfu ya askari wa Burundi nchini Somalia ifikapo Februari 28 mwaa huu, hatua ambayo serikali ya Burundi inailalamikia.

    Kwa upande wa serikali ya Burundi, kupelekwa kwa askari wake nchini Somalia ni katika hali ya kupata fedha.

    Serikali ya Burundi imekuwa ikishtumiwa kukwepesha sehemu ya mishahara, inayolipwa kwa dola na ambayo kwa kiasi kikubwa inatolewa na Umoja wa Ulaya.

    Marais wa Somalia na Burundi pia wameomba AMISOM kuendelea kusimamia mamlaka yake kamili. Pia wameahidi kuendesha operesheni dhidi ya kundi la wanamgambo wa Kiislamu la Al Shabab haraka iwezekanavyo, kwa kusubiri majeshi ya Somalia yajiimarishe.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako