• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (February 16-February 22)

    (GMT+08:00) 2019-02-22 18:59:17

    Juan Guaido, asema msaada wa dharura kutoka Marekani utaingia nchini Venezuela tarehe 23

    Kiongozi wa upinzani nchini Venezuela, Juan Guaido, ambaye hivi karibuni alijitangaza rais wa nchi hiyo, ametangaza kuwa msaada wa dharura kutoka Marekani utaingia nchini Venezuela tarehe 23 Februari licha ya rais Nicolas Maduro kukataa.

    Hivi karibuni rais Maduro alikanusha kuwa nchi yake haikabiliwi na njaa.

    Juan Guaido anasema hiyo itakuwa ni hatua ya kwanza kabla ya nchi yake kuingiliwa kijeshi.

    Ameomba watu 250,000 watakaojitolea kwa kusaidia katika kusafirisha misaada kutoka eneo inakofadhiliwa kwenye mpaka na Colombia hadi mjini Caracas, nchini Venezuela. Februari 23, itakuwa mwezi ni mmoja tangu Juan Guaido ajitangaze rais wa mpito wa Venezuela.

    Wakati huo huo Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergei Lavrov amemuonya mwenzake wa Marekani Mike Pompeo dhidi ya "matumizi yoyote ya nguvu" nchini Venezuela, wakati Washington ilisema iko tayari kuingilia kijeshi nchini Venezuela.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako