• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (March 23-March 29)

    (GMT+08:00) 2019-03-29 20:03:15

    Papa Francis asema kuzuia watu kubusu pete yake ni suala la kiafya na si vinginevyo

    Papa Francis amevunja kimya chake juu ya mkasa wa kuzuia waumini kubusu pete yake akisema lilikuwa ni suala la kiafya zaidi.

    Msemaji wa Vatican Alessandro Gisotti amesema kuwa Papa alikuwa akihofia kusambaa kwa vijidudu alipokuwa akikutana na waumini wa Kanisa Katoliki siku ya Jumatano.

    Wahafidhina ndani ya kanisa walipinga vikali kitendo hicho wakidai Papa anavunja utamaduni wa muda mrefu wa kanisa. Gisotti amesema kuwa kulikuwa na watu wengi waliokuwa kwenye msururu wa kumsalimia Papa na yeye akawa na tahadhari juu ya uwezekano wa kusambaza vijidudu.

    Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki mwenye miaka 82 anadaiwa "kufurahishwa" na utata huo, msaidizi wa Papa amewaambia waandishi wa habari.


    1  2  3  4  5  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako