Maandamano yakumba mpaka wa Kenya na Tanzania
Maandamano yamekumba mji wa mpakani wa Namanga uliopo kati ya kenya na Tanzania.
Kulingana na maafisa wa polisi maandamano hayo yalizuka kufuatia kutekwa nyara kwa mfanyibishara mmoja wa Kenya ambaye waandamanji hao wanasema alipelekwa nchini Tanzania.
Mfanyikazi wa ofisi ya serikali katika mji huo ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa waandamanaji hao waliojawa na ghadhabu walifunga barabara inayoelekea Tanzania na kukatiza uchukuzi kutoka na kuelekea nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |