Mwanamke anayedaiwa kuwa na mifuko miwili ya uzazi, ajifungua mapacha mwezi mmoja baada ya kujifungua mtoto wa kwanza
Mwanamke mmoja raia wa Bangladesh amejifungua mapacha wawili karibu mwezi mmoja baada ya kujifungua mtoto njiti,
Arifa Sultana,20, alijifungua mtoto wa kiume mwishoni mwa mwezi Februari, lakini siku 26 baadae alikimbizwa tena hospitalini baada ya kupata maumivu ya tumbo.
Madaktari waligundua kuwa bado ni mja mzito wa watoto mapacha katika mji wake mwingine wa mimba, kisha alifanyiwa upasuaji wa dharura.
Watoto wake wamezaliwa wakiwa na afya njema kisha wakaruhusiwa kwa kuwa hawakuwa na tatizo lolote. Siku 26 baadae, alilalamika kuumwa tumbo akakimbizwa kwenye hospitali nyingine na kujifungua mtoto mwingine.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |