• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (August 10-August17)

    (GMT+08:00) 2019-08-16 18:31:53

    Urais wa Tunisi wavutia wagombea 26

    Wagombea ishirini na sita wamekubaliwa kuwania katika uchaguzi wa urais ujao nchini Tunisia, kati ya majina 97 yaliyowasilishwa.

    Miongoni mwa wagombea hao kuna wanaume 24 na wanawake wawili. Wagombea ambao hawakukubaliwa wana muda hadi Agosti 31 ili kukata rufaa.

    Orodha ya wagombea hao imetangazwa na mamlaka inayohusika na uchaguzi, ISIE. Mamlaka hiyo imebaini kwamba wagombea hao 26 ndio wamekamilisha vigezo na masharti ya kuwania kiti cha urais.

    Kwa upande mwingine, majina yaliyotarajiwa yamekubaliwa, kama vile mwanzilishi wa kituo cha Televisheni cha Nessma TV, Nabil Karoui, Waziri Mkuu Youssef Chahed, naibu kiongozi wa chama cha Kiisilamu cha Ennahdha na Spika wa Bunge la Kitaifa Abdel Fatah Mourou, au Waziri wa Ulinzi, Abdelkarim Zbidi, mmoja kati ya wagombea wanaopewa nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi ambaye anatwania kama mgombea binafsi.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako