• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (August 10-August17)

    (GMT+08:00) 2019-08-16 18:31:53

    Burundi yazindua kampeni ya chanjo ya Ebola kwa wahudumu wa afya

    Wizara ya afya ya umma na kudhibiti ukimwi ya Burundi imezindua kampeni ya chanjo dhidi ya virusi vya Ebola kwa wahudumu wa afya na wasaidizi wengine wa karibu.

    Kwa mujibu wa shirika la afya ulimwenguni WHO njanyo hiyo ilianza rasmi Jumanne Agosti 13 kwenye eneo la Gatumba mpakani mwa Burundi na Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC.

    Kampeni hii ya chanjo ya Ebola ni sehemu ya maandalizi ya serikali ya Burundi kwa ajili ya uwezekano wa kuzuka kisa cha Ebola.

    Kampeni hii inatekelezwa chini ya usimamizi wa wizara ya afya ya umma na kudhibiti Ebola, kwa msaada wa shirika la afya duniani WHO. Na msaada wa kifedha wa kuendesha kampeni hiyo umetolewa na muungano wa chanjo duniani GAVI.

    Burundi imepokea dozi za chanjo ya Ebola aina ya rVSV-ZEBOV kuwalinda waauguzi hao dhidi ya virusi vya Ebola aina ya Zaire ambavyo imeiathiri DRc hivi sasa.

    Shirika la WHO linasema ingawa chanjo hiyo bado iko kwenye majaribio, haijaidhinishwa wala kuruhusiwa kuuzwa , imedhihirisha inafanya kazi na ni salama wakati wa mlipuko wa Ebola uliozuka Afrika Magharibi na utafiti zaidi unahitajika kabla haijaidhinishwa na kupewa leseni.

    WHO inasema chanjo hiyo inatolewa kwa sababu za kibinadamu , kuwalinda wahudumu wa afya na walio msitari wa mbele katika hatari zaidi ya kuambukizwa mlipuko ukizuka na kwenye maeneo yaliyo na hatari zaidi ya maambukizi.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako