• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (27 Juni-1 Julai)

    (GMT+08:00) 2016-07-01 17:23:00

    Rodrigo Duterte aapishwa kuwa rais mpya wa Ufilipino

    Rais mpya wa Ufilipino Rodrigo Duterte ameapishwa rasmi wiki hii na jaji wa mahakama kuu kwenye hafla iliyofanyika katika ikulu ya nchi hiyo.

    Baada ya kuapishwa, Duterte ambaye anakuwa rais wa awamu ya 16 alitoa hotuba fupi.

    Habari nyingine zinasema, rais Xi Jinping wa China amemtumia salamu za pongezi rais Duterte akisema, anataka kufanya juhudi pamoja na rais huyo ili kuboresha uhusiano kati ya nchi hizi mbili na kutimiza maendeleo endelevu.

    Tarehe 9 Mei mwaka huu, uchaguzi mkuu ulifanyika nchini Ufilipino ambapo Bw. Duterte akiwa meya wa mji wa Davao alipata ushindi kwa kupata kura zaidi ya milioni 16.6, na kipindi cha urais wake ni miaka 6.

    -

    1 2 3 4 5 6 7 8 9
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako