Watu 10 wakamatwa kwa tuhuma za ugaidi Brazil
Polisi nchini Brazil imewatia mbaroni watu 10 wanaodaiwa kuwa wafuasi wa kundi lenye itikadi kali la Dola la Kiislamu.
Watuhumiwa wanadaiwa walikuwa wanapanga mashambulizi katika kipindi cha michezo ya Olimpiki mjini Rio de Janeiro.
Waziri wa Sheria wa Brazil Alexandre de Moraes amesema kundi hilo lenye kujumuisha Wabrazil wengi limeripotiwa likifanya mjadala wa kununua silaha na kuifanya mbinu za vita vya msituni katika kutekeleza azma yao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |