Erdogan atangaza kulifanyia mageuzi jeshi la Uturuki
Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki ametangaza wiki hii kulifanyia mabadiliko jeshi la nchi hiyo hatua ambayo inachukuliwa si zaidi ya wiki moja baada ya tukio la mapinduzi lililoshindwa.
Hayo yanajiri wakati kukionekana uwezekano wa kutokea uasi miongioni mwa maafisa wa jeshi.
Akizungumza katika mahojiano yake na shirika la habari la Uingereza, Reuters, Erdogan amesema wamekuwa macho zaidi. Baada ya jaribio la mapinduzi maelfu ya wanajeshi na maafisa walikamatwa.
Serikali ya Ankara imewatuhumu waasi wenye kuhusiana na mtandao wa mhubiri wa Kituruki anayeishi uhamishoni Marekani Fethullah Gulen.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |