• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii ( Agusti 6-Agusti 12)

    (GMT+08:00) 2016-08-12 18:25:13
    Erdogan aahidi ushirikiano na Urusi

    Rais Vladimir Putin wa Urusi na mwenzake wa Uturuki Recep Erdogan wiki hii wameahidi kuimarisha uhusiano wao baada ya mkutano wao wa kwanza tangu Uturuki ilipoiangusha ndege ya Urusi Novemba mwaka jana.

    Uturuki wakati huo huo imeuonya Umoja wa Ulaya kwamba unafanya makosa makubwa katika mtazamo wake kuhusu jaribio lililoshindwa la mapinduzi nchini humo.

    Erdogan alifanya ziara hiyo katika mji alikozaliwa rais Putin wa St. Petersburg ikiwa pia ya kwanza nje ya nchi yake tangu pale lilipofanyika jaribio lililoshindwa la mapinduzi dhidi yake mwezi uliopita ambalo lilizusha msako mkubwa dhidi ya wapinzani na kuweka kiwingu katika uhusiano kati ya Uturuki na mataifa ya magharibi.


    1 2 3 4 5 6 7 8 9 10
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako