• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii ( Agusti 6-Agusti 12)

    (GMT+08:00) 2016-08-12 18:25:13

    Ujerumani yachukua hatua kali zaidi za kupambana na ugaidi

    Waziri wa mambo ya ndani wa Ujerumani Thomas De Maiziere ametangaza hatua kadhaa za kupambana na ugaidi.

    Hatua hizo ni pamoja na kuongeza askari 4600 wa usalama, kuimarisha mapambano dhidi ya ugaidi na ushirikiano ndani ya Umoja wa Ulaya, kudhibiti vibali vya kuishi kwa wageni ambao walikuwa na rekodi ya uhalifu.

    Bw. De Maiziere ameeleza kuwa, mpango huo unalenga kuimarisha kikosi cha usalama, kukinga mashambulizi kabla hayajatokea, kusaidia wakimbizi kujiunga na jamii, na kuwaadhibu wahalifu.

    Hatua hiyo inakuja baada ya mashambulizi ya mfulululizo yaliyotokea mwezi uliopita nchini humo. Mpaka sasa, polisi wa Ujerumani imetangaza kuwakamata watuhumiwa wanne wanaoshukiwa kuwa na uhusiano na kundi la IS.


    1 2 3 4 5 6 7 8 9 10
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako