Umoja wa Afrika waanza tena mchakato wa kuteua wajumbe wa kamati yake
Wiki hii Umoja wa Afrika umeanza tena mchakato wa kuchagua mwenyekiti, naibu mwenyekiti na wajumbe wanane wa awamu ijayo wa kamati ya Umoja huo.
Kamati ya Umoja wa Afrika imetoa taarifa rasmi kwa nchi wanachama wote, na kutoa ratiba na muda wa mwisho wa kuwasilisha wagombea wa nafasi hizo 10.
Mchakato huu unawaruhusu wagombea wapya na wa zamani ambao walishindwa kupata kura za kutosha kwenye uchaguzi uliofanyika wakati wa mkutano wa Kamati hiyo mjini Kigali, Rwanda, kushiriki katika uchaguzi huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |