• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii ( 9 Desemba-15 Desemba)

    (GMT+08:00) 2017-12-15 18:03:15

    Mnangagwa aomba Zimbabwe iondolewe vikwazo

    Rais mpya wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa, ametoa wito wa kuondolewa vikwazo vilivyowekwa na mataifa ya magharibi dhidi ya taifa hilo.

    Kadhalika, amesema kwamba huenda uchaguzi ulioratibiwa kufanyika Julai mwaka ujao ukafanyika mapema.

    Akizungumza na viongozi wa chama tawala cha ZANU-PF, Bw Mnangagwa amesema vikwazo hivyo vinalemaza ufanisi wa taifa hilo, na kusema vinafaa kuondolewa bila masharti yoyote.

    Amesema serikali ya taifa hilo itahakikisha kwamba uchaguzi umefanyika kwa njia huru na haki.

    Bw Mnangagwa alichukua uongozi mwezi jana baada ya Robert Mugabe aliyekuwa ameongoza taifa hilo kwa miaka 37 kuondolewa madarakani kwa usaidizi wa jeshi.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako