• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii ( 9 Desemba-15 Desemba)

    (GMT+08:00) 2017-12-15 18:03:15

    Maonesho ya kwanza ya ushirikiano wa nishati kati ya China na Afrika yatafuta maendeleo ya pamoja

    Maonesho ya kwanza ya ushirikiano wa nishati kati ya China na Afrika yamefunguliwa mjini Nairobi, yakishirikisha viwanda takriban 60 vya China kuonesha teknolojia na vifaa vya kisasa za China katika sekta za ujenzi wa miundo mbinu, mitambo, na upashanaji wa habari, ili kuimarisha ushirikiano kati ya pande hizo mbili na kutafuta maendeleo ya pamoja.

    Mkuu wa ujumbe wa China kwenye maonesho hayo Bw. He Cailong ameeleza kuwa, hii ni hatua muhimu katika kutekeleza mipango kumi ya ushirikiano kati ya China na Afrika, na makubaliano yaliyowekwa kwenye Mkutano wa viongozi wa Baraza la ushirikiano wa kimataifa kuhusu "Ukanda mmoja, Njia moja", na kusukuma mbele ushirikiano wa kimataifa katika sekta za nishati na utengenezaji wa vifaa.

    Waziri wa ushirikiano wa viwanda na biashara Bw. Adan Mohamed amesema maonesho hayo yameonesha kuwa uhusiano na ushirikiano kati ya China na Afrika unazidi kupata maendeleo.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako