• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Mei 5-Mei 11)

    (GMT+08:00) 2018-05-11 18:46:31

    Kenya yaimarisha doria uwanja wa ndege baada ya ebola kuripotiwa DRC

    Serikali ya Kenya imeimarisha doria katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Jomo Kenyatta na vituo vingine vya mpakani baada ya visa vya ugonjwa wa Ebola kuripotiwa kaskazini magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

    Kuna visa viwili vilivyothibitishwa kwa sasa, wizara ya afya ya DR Congo imethibitisha.

    Watu 17 walikuwa wameripotiwa kufariki kutokana na ugonjwa usiojulikana, ambao unadhaniwa kuwa Ebola eneo hilo.

    Waziri wa Afya Kenya Bi Sicily Kariuki amesema wasafiri wote wanaofika uwanja wa ndege wa JKIA na vituo vya mpakani vya Busia na Malaba watakuwa wakipimwa viwango vyao vya joto mwilini.

    Nigeria pia imeimarisha doria mpakani.

    Wataalam wa maradhi ya Ebola kutoka wizara ya afya nchini DR Congo wanatarajiwa kuambatana na wale wa shirika la afya duniani WHO kwenda jimboni Equateur baada ya kuthibitishwa kuwepo kwa visa hivyo.

    Kisa kilichotokea katika mji wa Bikoro kinajiri zaidi ya mwaka baada ya mlipuko wa ugonjwa huo kusababisha vifo vya watu wanne nchini humo.

    Mnamo 2014 zaidi ya watu 11,000 waliuawa nchini Guinea, Sierra Leone na Liberia.

    Hii ni mara ya tisa kunazuka ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

    Virusi vya ugonjwa huo viligunduliwa kwa mara ya kwanza katika nchi hiyo iliyokuwa ikijulikana kama Zaire, mnamo 1976 na jina lake linatokana na mto Ebola.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako