• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Agosti 25-Agosti 31)

    (GMT+08:00) 2018-08-31 20:50:29

    Ghasia za ubaguzi zaibuka tena nchini Afrika Kusini

    Ghasia za ubaguzi zaibuka tena nchini Afrika Kusini

    Ghasia za ubaguzi zimeibuka tena nchini Afrika Kusini, hasa katika maeneo mengi ya Soweto. Watu wawili waliuawa katika mapigano yaliyotokea kati ya wenyeji na wageni katika mji wa Soweto, kwa mujibu wa polisi.

    Shughuli katika maeneo mengi ya Soweto zilizorosta, huku maduka yanayomilikiwa na wageni yakiporwa bidhaa kufuatia ghasia hizo.

    Idadi ya maduka haya yanayomilikiwa na wageni yamejengwa katika maeneo ya karibu na makazi na yamekuwa yakimilikiwa raia pia kutoka nchi nyingine kama vile Ethiopia, Zimbabwe na Pakistan.

    Hali hiyo pia imewafanya wamiliki wengi wa maduka kufungasha bidhaa zao na kuondoka mjini humo wakihofia vurugu zaidi.

    Kwa mujibu wa polisi ghasia hizo zilianzia katika duka moja, baada ya wakazi wa eneo hilo kumtuhumu mmiliki wa duka mwenye asili ya Somalia kumshambulia kwa risasi na kumuua kijana mdogo aliyedai kuwa alikuwa akijaribu kuvunja duka lake.

    Wakazi hao pia wanawalaumu wamiliki wa maduka, ambao wengi ni wageni, kuuza vyakula vilivyopitwa na wakati.

    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako