• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Agosti 25-Agosti 31)

    (GMT+08:00) 2018-08-31 20:50:29

    Zambia kukabiliwa na ongezeko la wakimbizi kutoka DRC

    Zambia inatarajiwa kuwa na ongezeko la idadi ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kabla ya mwisho wa mwaka huu.

    Kamishna anayeshughulikia mambo ya wakimbizi wa wizara ya mambo ya ndani ya Zambia Bw. Abdon Mawere amesema tayari Zambia imeanza kushuhudia ongezeko la idadi ya wakimbizi.

    Akiongea kwenye mkutano mmoja wa wadau wa suala la wakimbizi Bw. Mawere amesema hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu, Zambia inatarajiwa kupokea wakimbizi elfu 76, na serikali itaanza kuwahusisha wakimbizi kwenye mipango ya taifa, ili kuwafanya wanufaike na huduma za jamii.

    Mwakilishi wa Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR nchini Zambia, Bw. Pierrine Aylara, amesema juhudi za makusudi zinatakiwa kufanyika, ili kuisaidia serikali ya Zambia kukabiliana na tatizo la wakimbizi.

    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako