• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Agosti 25-Agosti 31)

    (GMT+08:00) 2018-08-31 20:50:29

    Rais wa Zimbabwe aunda tume kuchunguza vurugu zilizotokea kwenye uchaguzi mkuu wa Zimbabwe

    Rais Emerson Mnangagwa wa Zimbabwe ametangaza kuunda tume ya watu saba kuchunguza vurugu zilizotokea wakati wa uchaguzi mkuu wa nchi hiyo, na kusababisha vifo vya watu sita.

    Tume hiyo itakayoundwa na wenyeji, watu kutoka kanda hiyo na nje ya kanda hiyo, itakuwa chini ya uenyekiti wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Bw Kgalema Motlanthe, na inatarajiwa kuwasilisha ripoti yake miezi mitatu baada ya kuapishwa kwa Rais Mnangangwa.

    Walioko kwenye tume hiyo ni pamoja na Rodney Dickson kutoka Uingereza, aliyekuwa katibu mkuu wa jumuiya ya madola Bw Emeka Anyaoku kutoka Nigeria, na aliyekuwa mkuu wa majeshi wa Tanzania, Jenerali Davis Mwamunyange.

    Bw. Mnangagwa amesema amesikitishwa na vifo hivyo na kukilaumu chama cha upinzani cha MDC kwa vurugu hizo, na waangalizi wa uchaguzi wamelilaumu jeshi.

    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako